Description
“Halima mwanangu, wakati mwingine nashindwa kuelewa dunia inaelekea wapi. Visa kama hivyo ni vingi tu katika maisha yetu siku hizi. Ajabu ni kuwa, licha ya madhalimu hao kufikishwa mbele ya sheria, wao hufanya hila wakajipa uhuru.” Matumaini ya familia ya Halima yanafufuka pale anapopata ajira kama mjakazi. Kwake Halima, anaiona fursa hii kuwa muhimu zaidi katika kutimiza maazimio yake na ndoto zake maishani. Maisha yanamwia mazuri Dar es Salaam hadi siku moja ambapo mambo yanaharibika na kumtia wasiwasi kuhusu mipango yake na mchumba wake. Je, ni mambo gani yaliharibika, na nani kayaharibu?
‘Pigo la Nafsi’ ni hadithi inayosimuliwa kwa upekee wa namna yake. Hadithi hii imejaa mafunzo yanayoakisi uhalisia wa maisha, katika dunia ya sasa.
Reviews
There are no reviews yet.