Description
Tajriba yangu imenifundisha kuwa kila binadamu ni mlemavu, lakini ulemavu si kutojiweza. Kila binadamu ana uwezo fulani ambao unahitaji kutambuliwa na kurutubishwa. ‘Ulemavu pekee niujuao ni wa fikra na mielekeo hasi; si wa maumbile …’
Mwandishi, Godfrey Ipalei, alizaliwa mikono yote miwili ikiwa nusunusu. Licha ya hayo, amesoma katika shule za kawaida hadi chuo kikuu na kuajiriwa kazi, ambayo kwa kawaida angeonekana kutoiweza. Ipalei ameweza kufanya mengi ambayo hayangetarajiwa katika hali yake. Kwa sasa, yeye ni
mtaalamu wa tarakilishi katika Shirika la Huduma kwa Wanyamapori, Kenya (KWS).




Reviews
There are no reviews yet.